Posts

Showing posts from August, 2017

SHIRIKA LA POSTA LAKUSANYA SHILINGI BILIONI 7.6 ZA MADENI

Image
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu Mhe. Prof. Norman Sigala King (katikati), akiongoza kikao cha Kamati yake na Shirika la Posta Tanzania (TPC), kilichofanyika mjini Dodoma. Kulia ni Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani na kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Moshi S. Kakoso. Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng.  Edwin Ngonyani, akifafanua jambo kwa  Kamati ya Bunge ya Miundombinu  katika kikao chao na Shirika la Posta Tanzania (TPC), kilichofanyika mjini Dodoma. Kulia ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Prof. Norman Sigala King na kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Sekta ya Mawasiliano Eng. Angelina Madete. Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC), Luteni Kanali mstaafu Haruni Kondo, akitoa taarifa ya Shirika hilo kwenye kikao chao na Kamati ya Bunge ya Miundombinu kilichofanyika mjini Dodoma. Kulia kwake ni mjumbe wa Kamati hiyo Mhe. Anna Lupembe. Mjumbe wa Kama...

SERIKALI YA MAREKANI YAREJEA UPYA AHADI YAKE YA KUFANYA KAZI NA JESHI LA WANANCHI WA TANZANIA KATIKA MAPAMBANO DHIDI VVU/UKIMW

Image
Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania Dr. Inmi Patterson na Mkuu wa Huduma za Kitabibu wa JWTZ, Meja  Generali (Dk.) Denis Raphael Janga wakitiliana sini mkataba wa kitabibu kwa ajili ya huduma za matibabu ya VVU/UKIMWI nchini Tanzania. Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania Dr. Inmi Patterson na Mkuu wa Huduma za Kitabibu wa JWTZ, Meja  Generali (Dk.) Denis Raphael Janga wakibadilishana nyaraka mara baada ya kusaini kwa ajili ya huduma za matibabu ya VVU/UKIMWI nchini Tanzania. Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania Dr. Inmi Patterson na Mkuu wa Huduma za Kitabibu wa JWTZ, Meja  Generali (Dk.) Denis Raphael Janga wakipiga picha ya pamoja na maofisa wa Ubalozi wa Marekani na Jeshi la Wananchi JWTZ mara baada ya kusiniana mkataba huo. ……………………………………………………………………………………….  Serikali ya Marekani kupitia Taasisi ya kijeshi ya  Walter Reed  (WRAIR) imesaini upya makubaliano ya ushirikiano na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) siku ya Ju...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

Image
Sambaza habari hii Facebook   Sambaza habari hii Twitter   Sambaza habari hii Messenger   Sambaza habari hii Email   Mshirikishe mwenzako Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Kore...

MAONESHO YA WAANDISI KUFANYIKA MJINI DODOMA

Image
 Kaimu wa Bodi ya usajili wa Waandisi nchini Muhandisi Patrick Barozi Timothy Marko. KATIKA kutathimini mchango wa Waandisi nchini jumuhia ya Waandisi inatarajia kuadhimisha siku ya waandisi september 7 Mwaka huu katika ukumbi wa Jakaya KIKWETE Convetion center uliopo mjini Dodoma . Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es salaam Kaimu wa Bodi ya usajili wa Waandisi nchini Muhandisi Patrick Barozi amesema kuwa maadhimisho hayo yataendana sambamba na kiapo cha watalamu wa uhandisi na maonesho mbalimbali ya kifundi na biashara pamoja nakuwazawadia waandisi wahitimu waliofanya vizuri mitihani ya kuhitimu uhandisi katika kipindi cha mwaka 2016/17. ''Maadhimisho ya mwaka huu yataendana na taasisi mbalimbali kuonesha bidhaa zikiwemo mashine mbalimbali ikiwemo mashine za kushindilia barabara zilizogunduliwa nawatalamu wa kitanzania sambamba na mashine ya kuchakata migomba nakutengeneza nywele za bandia za kinadada ,mashine yakusaga mihogo pamoja namashine za power ...

ARSENAL YAKUBALI YAISHI KWA SANCHEZ SASA KUTUA MAN CITY WAKATI WOWOTE

Image
Inavyoelekea timu ya Arsenal sasa iko tayari kumuachia mshambuliaji wao hatari Alexis Sanchez kujiunga na  Manchester City,Lakini sharti lake ni kulipwa pauni milioni 70 na mshambuliaji Raheem Sterling. Awali, Man City ilikuwa kutoa pauni milioni 50 na Sterling. Lakini Kocha Arsenal Wenger akasema watoe fedha hizo pamoja na mshambuliaji Kun Aguero, Man City nao hawakukubaliana nalo. Hata hivyo kinachoonekana baada ya muda klabu hizo zitaelewana kabla ya dirisha kufungwa kesho saa sita usiku.

SERIKALI YAVITAKA VYOMBO VYA HABARI KUACHA UCHOCHEZI

Image
Timothy Marko SERIKALI nchini Tanzania imevionya Baadhi ya vyombo vya Habari vinavyokiuka maadili ya uandishi wa Habari kwa kuandika habari zinazochochea nakuleta mtafaruku kwa jamii Onyo hilo limekuja baada ya Gazeti la Nipashe kuandika kichwa cha habari kisemacho'' NIMATESO ''toleo la leo  sambamba nagazeti la MWANANCHI lenye kichwa cha habari Bomoa Bomoa nyingine yakufa mtu yaja Dar ''ambapo serikali imedaikuwa vyombo hivyo vimekuwa vikichochea na kuleta taharuki kwa jamiii. Akizungumza nawaandishi wa Habari jijini Dar es salaam  Mkurugezi mkuu wa idara ya Habari na Msemaji waserikali Hassan Abbas amesemakuwa vichwa vilivyotolewa namagazeti hayo vimekiuka misingi yahabari ambapo vinamtaka kutohukumu wa kati wakuandika habari yoyote . ' 'VICHWA HIVI VIMEKIUKA MISINGI Ya habari ikimewemo kuhukumu yani judgemental headline uandishi wahabari unaosimimia haki naukweli nimsingi kwajamii yetu''Alisema HASSAN ABASS

DSTV LATANGAZA PUNGUZO LA BEI YA VINGA'MUZI

Image
bukuku 3 mins ago BIASHARA Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice Tanzania Maharage Chande na Balozi wa Multchoice Nancy Sumari wakikabidhi zawadi kwa washindi baada ya kushindwa katika bahati nasibu wakati wakitangaza punguzo kubwa la bei kwa vifurushi vyote vya DStv bei zitakazoanza kutumika rasi Septemba mosi 2017. Balozi wa Multchoice Tanzania Nancy Sumari akizungumza mara baada ya kutagazwa kwa punguzo kubwa la vufurushi wa DSTV leo. Punguzo linavyoonekana katika kipeperushi Meneja Masoko wa Multchoice Tanzania Bw. Alfa Mria akizungumza katika hafla hiyo ya kutangaza punguzo kubwa katika vifurushi vyote vya DSTV. Meneja Mawasiliano wa Multchoice Tanzania Bw. Jonson Mshana akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha Mkurugezi Bw. Maharage Chande kwa ajili ya kutangaza punguzo la vifurushi hivyo. Baadhi ya wafanyakazi wa Multchoice Tanzania wakiwa katika hafla hiyo Afisa Masoko na Mawasiliano wa Mult...

Korea Kaskazini yarusha kombora juu ya anga ya Japan

Image
Korea kaskazini imerusha makombora yake ambayo yalipita Japan kabla ya kudondokea baharini. Makombora hayo yalisafiri kuelekea mashariki karibu kilomita elfu moja juu ya kisiwa cha Japan cha Hokkaido. Tukio hilo limechochea tahadhari ya hatari ambayo watu walielekezwa kujificha katika maeneo yaliyo chini ya ardhi ama kwenye majengo yaliyo imara. Waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe amesema urushwaji huo wa makombora ambao haujawahi kutokea , umeleta kitisho kikubwa kwa taifa lake Wanajeshi wa Marekani na Japan wanafanya zoezi la pamoja katika eneo hilo la Hokkado, rais wa Korea Kusini Moon Jae-in aliagiza uwezo wa utumiaji wa nguvu ili kujibu shambulio hilo. Ndege nne za Korea Kusini zilifanya zoezi la kurusha makombora siku ya Tuesday. Bwana Abe alisema kuwa amezungumza na rais wa Marekani Donald Trump na kwamba wote wamekubaliana kuiongezea shinikizo Korea Kaskazini. Katika mfululizo wa majaribio yake ya makombora ya hivi karibuni Korea kaskazini haijawahi kurusha mak...

TFF YAIFANYIA MAREKEBISHO NGAO YA JAMII WALIOICHUKUA SIMBA

Image
  Hatimaye Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limefanya marekebisho katika Ngao ya Jamii waliyoshinda Simba. Simba walikabidhiwa Ngao ya Jamii baada ya kuifunga Yanga kwa mikwaju 5-4 ya penalti, lakini ikawa na makosa katika maandishi. Ngao hiyo ilikuwa imeandikwa, Community Sheild badala ya Community Shield. Baada ya malalamiko kuwa makubwa, TFF iliomba Simba kuirudisha ngao hiyo kwa ajili ya marekebisho na sasa hilo, limefanyika.  

NIC Bank Yakabidhi Magari Matatu kati ya Sita Kwa Mteja wake kama Mkopo

Image
Meneja mahusiano kwa wateja wakubwa wa benki ya NIC Tanzania, Woinde Murro(kulia) akizungumza jambo na mmoja wa wateja waliofika kwaajili ya kukabidhiwa magari makubwa ikiwa awamu ya kwanza ya mkopo wa Magari Sita ambapo leo amepokea magari matatu na matela matatu Meneja mahusiano kwa wateja wakubwa wa benki ya NIC Tanzania, Woinde Murro(kulia)  akimkabidhi funguo  Mkurugenzi wa kampuni ya Usafirishaji ya Simera, Bw.Zainul Dossa(kushoto) za magari matatu waliyokopeshwa na Benki ya NIC Meneja Uendeshaji kutoka Kampuni ya Usafirishaji ya Simera, Bw. Arif akiwasha moja ya gari mara baada ya Benki ya NIC kukopesha magari sita kwenye kampuni ya Usafirishaji ya Simera leo jijini Dar es Salaam. Magari matatu kati ya sita yalikabidhiwa na benki ya NIC kama mkopo kwa mteja wao Leo benki ya NIC imekabidhi magari makubwa matatu na matela yake kati ya magari sita ambayo yamekabidhiwa kama mkopo kwa Mteja wao Simera. Makabidh...

TANROADS TABORA KUTEKELEZA AGIZO LA JPM UJENZI WA BARABARA ZILIZOBAKI

Image
Na Tiganya Vincent RS-TABORA 29 AUGUSTI 2017 WAKALA  wa Barabara nchini ( TANROADS )  mkoani Tabora imesama kuwa tayari imeshaanza kutekeza hatua mbalimbali za maandalizi ya ujenzi wa barabara ambazo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli aliagiza ujenzi wake uanze mara moka wakati akiwa katika ziara ya mkoa huo. Kauli hiyo ilitolewa jana mjini Tabora na Meneja wa TANROADS Mhandisi Damian Ndabalinze kwenye kikao kazi kiliandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora kwa Mameneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mjini Tanzania( TARURA) wa mkoani humo.  Mhandisi Ndabalinze alisema kuwa katika barabara ya kutoka Kaliua hadi Urambo kazi za awali za kwa ajili ya kuanza maandalizi ya ujenzi inaendelea katika eneo la mradi. Alisema kwa upande wa barabara ya ujenzi wa barabara ya Nyahua hadi Chaya yenye urefu wa Kilometa 84 wameshaanza hatua za awali baada ya Kuwait Fund ambaye ndio watoa fedha za mko...

JESHI LA POLISI KUENDELEA NA UCHUNGUZI KULIPULIWA OFISI ZA MAWAKILI DAR

Image
Kamishina wa polisi Msaidizi wa Kanda Maalum DA(SAP) Lazaro MAMBO SASA Timothy Marko  JESHI la Polisi kanda Maalum jijini Dar es salaam limesema linaendelea kufanya uchunguzi wa kisayansi juu ya kuwepo kwa taarifa za kulipuliwa kwa ofisi za Mawakili wa kujitegemea jijini hapa kwakuwahusisha watalamu mbalimbali wa milipuko . Akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es salaam Kamishina wa polisi Msaidizi wa Kanda Maalum(SAP) Lazaro Mambosasa amesema kuwa jeshi hilo linaendelea na utafiti wa kisayansi ilikuweza kubaini nini chanzo cha Mlipuko huo nakuwataka wananchi kutoa ushirikiano na jeshi hilo pindi watakapo hitaji taarifa . ''tumelipokea taarifa za kulipuliwa kwa ofisi za mawakili nasuala hili lipo katika upelelezi tishio hili linahusianisha uchanganuzi wakisayansi hivyo tunawataka wananchi kutoa ushirikiano ''Alisema Lazaro Mambo sasa  Mambo sasa aliwataka wananchi kutokurupuka kuhusiana na tukio hilo nakuwataka kuwa watulivu kusiana nasuala hilo nak...

PITIA VICHWA VYA HABARI VYA MAGAZETI

Image