Adebayo Akinfenwa: Sergio Ramos ana bahati hatutakutana uwanjani
\MTADAO WA BBC Mshambuliaji wa klabu ya Uingereza ya Wycombe Wanderers Adebayo Akinfenwa ametoa onyo kali kwa nahodha wa Real Madrid Sergio Ramos. Ramos amekuwa akishutubiwa baada ya nyota wa Liverpool na Misri Mohamed Salah kuumia begani walipokabiliana wakati wa fainali ya Kombe la Klabu Bingwa Ulaya. Ramos pia aligongana na kipa wa Liverpool Loris Karius na inadaiwa kwamba huenda tukio hilo lilimduwaza kwa kumsababishia mtikisiko wa ubongo jambo ambalo pengine lilichangia makosa ya kushangaza aliyoyafanya kipa huyo. Makosa yake mawili yalichangia mabao mawili ya Real Madrid ambao walishinda mechi hizo 3-1. Sergio Ramos afunguka kuhusu kuumia kwa Mo Salah Akinfenwa ameandika kwenye Twitter kwamba daima atakuwepo kuwasaidia na kuwaunga mkono Liverpool wakitishiwa. Amepakia video kwenye mtandao huo wa kijamii akionesha nguvu zake kwa kuvuta buti kwa kutumia mikono yake mwenyewe. Klabu yake inatokea High Wycombe eneo la Buckinghamshire, England na inachez...