Posts

Showing posts from April, 2018

SERIKALI YATOA UFAFANUZI JUU YA MAPATO KATIKA SEKTA YA MADINI .

Image
WAZIRI WA MADINI ANGELA KAIRUK I Timothy Marko  SERIKALI imesema katika kipindi cha mwaka wa fedha2015/16 zaidi ya shilingi bilioni 434.6 zimeweza kupatikana kutokana na tozo ya kodi katika sekta ya madini na gesi amabapo jumla ya kampuni 55zinazojishulisha nauchimbaji mafuta nagesi ziliweza kutozwa kodi kwenye sekta hiyo . Akizungumza katika mkutano wa uzinduzi wa ripoti ya nane ya taasisi ya uhamasishaji wa  uwazi na uwajibikaji wa rasmali za madini mafuta na gesi asilia jijini Dar es salaam Waziri wa madini Angela Kairuki amesema kuwa sambamba namapato hayo katika ripoti hiyo ilionesha kuwa baadhi ya makampun yamekuwa yakilipa zaiodi ya shilingi bilioni465 .1 hali iliyochangia utofauti wa zaidi ya shilingi bilioni 30.5 ambayo nipungufu . ''Ninaeleza kuwa taarifa hii  ipelekwe kwa mkaguzimkuu wa mahesabu ya serikali kama ilivyo anishwa katika kifungu cha 18 (1)katika ripoti hii imeonesha kuwa sekta ya madini imeonesha kuwaji wa asilimia 85 katika ukuwaji...

WAZIRI UMMY ALIA NA VIONGOZI WADINI JUU YA SARATANI .

Image
Waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Ummy Mwalimu Timothy Marko. SERIKALI imewataka viongozi wadini kuwahamasisha wauminiwao katika nyumba mbalimbali za ibada juu uanzishwaji wa chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi itakayo wahusu wasichana wenye umri kati ya miaka 14 nakuendelea itayoendeshwa nchi nzima nakusisitiza kuwa chanjo hiyo haina madhara ya kiafya kama ilivyo kaririwa na baadhi yawatu . Akizungumza katika kongamano lililowakutanisha viongozi wadini jijini Dar es salaam Waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Ummy Mwalimu amewataka viongozi wadini kuwahimiza waumini wao wakiwemo wazazi na walezi kuwa himiza wasichana wenye umri kati miaka14 nakuendelea kufika katika vituo vya afya ilikuweza kupata chanjo hiyo . ''Ninawaomba viongozi wadini mtusaidie kufikisha ujumbe wa uanzishwaji wa uanzishwaji wa chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi kwa mabinti wa miaka 14 iliwawezekukingwa dhidi ya madhara yanayoweza kuwapat...

Tetesi za Soka Ulaya

Image
Chelsea wanatarajia kumteua kocha wa Juventus, Massimiliano Allegri, kuwa meneja wa mpya mwishoni mwa msimu lakini kama itashindikana mazungumzo na meneja wa zamani wa Barcelona Luis Enrique. (Star) Klabu ya Real Sociedad ya nchini Hispania, inayosuasua kwenye ligi ya nchini humo inamtaka meneja wa Newcastle Rafael Benitez kuwa meneja wake mpya. (Mirror)

Wateja 676 wa Tigo wajinyakulia simu janja za TECNO R6 na bonasi za intaneti bure baada ya kununua bando za intaneti kupitia *147*00#

Image
Meneja Mawasiliano wa Tigo, Woinde Shisael (kushoto) na Mtalaam wa Bidhaa wa Tigo,   Jacqueline Nnunduma  (kulia) wakiongea na waandishi wa habari katika hafla ya kukabidhi zawadi za simu janja aina ya Tecno R6 kwa washindi wa promosheni inayoendelea ya Nyaka Nyaka Bonus. Tigo imetoa jumla ya simu 676 bure pamoja na bonasi za intaneti hadi GB 1 kwa wateja wake walionunua bando za intaneti kupitia menu yake iliyoboreshwa ya *147*00#.  Meneja Mawasiliano wa Tigo, Woinde Shisael (aliyesimama kulia) akimkabidhi Gladness Mori (alieyeketi) zawadi ya simu janja aina ya Tecno R6 aliyoshinda katika promosheni inayoendelea ya Nyaka Nyaka Bonus huku akitazamwa na baadhi ya washindi wengine wa promosheni hiyo. Tigo imetoa jumla ya simu 676 bure pamoja na bonasi za intaneti hadi GB 1 kwa wateja wake walionunua bando za intaneti kupitia menu yake iliyoboreshwa ya *147*00#.  Meneja Mawasiliano wa Tigo, Woinde Shisael (aliyesimama...

CAF YAWAZUIA YONDAN, TSHISHIMBI, CHIRWA NA MAKAPU KUCHEZA DHIDI YA WAHABESHI JUMAMOSI

Image
Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limeitumia barua ya tahadhari Yanga kutowatumia wachezaji wake wanne, mabeki Kelvin Yondan, Said Juma ‘Makapu’, kiungo Mkongo Papy Kabamba Tshishimbi na mshambuliaji Mzambia Obey Chirwa katika mchezo wa Jumamosi dhidi ya Welaita Ditcha ya Ethiopia.   Yanga watakuwa wenyeji wa Waleita Ditcha ya Ethiopia katika mchezo wa kwanza wa mchujo wa kuwania tiketi ya kucheza hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika Jumamosi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Na barua iliyoandikwa jana kutoka makao makuu ya shirikisho, Cairo nchini Misri imesema wanne hao pamoja na wachezaji wawili wa Welaita Ditcha, Teklu Tefesse Kumma na Eshetu Mena Medelecho hawaruhusiwi kucheza mechi hiyo baada ya kuonyeshwa kadi mbili za njano kila mmoja katika mechi zilizopita za timu zao.   Lakini Meneja wa Yanga, Hadidh Saleh amesema ni kweli wanafahamu Makapu, Tshishimbi na Chirwa wana kadi mbili za njano, lakini kw...

Gavana atuhumiwa kwa ubakaji DRC

Image
Naibu Gavana wa jimbo la Ikweta kusini magharibu nchini Jamuhuri ya demokrasia ya Congo ,Tathy Bikamba ameshtakiwa kwa tuhuma za ubakaji wa binti wa miaka 20 ambaye inadaiwa kuwa alimfanyia unyama huo baada ya kumpa dawa za kulevya. Gavana huyo anatarajiwa kufikishwa kinshasa kujibu tuhuma hizo mahakamani , ingawa wakili wake ametupia mbali tuhuma hizo.   Taarifa kutoka duru za karibu za uchunguzi wa kesi hiyo ya kubaka vinasema kwamba gavana huyo alimbaka binti huyo siku ya Jumamosi. Bwana Bikamba ambaye kwa sasa yuko gerezani anatarajiwa kufikishwa mahakamani hii leo ili aweze kujibu mashtaka yake ya kumwekea dawa ya kulevywa na kumfanyia tendo la ngono binti bila idhaa yake. Wakili wa gavana huyo, Imbambo Engulu ametupilia mbali tuhuma hizo na kushutumu mahakama ya jimbo hilo kwa kumzuia gavana huyo bila kujali na cheo chake "Kushikwa kwake ni kama uonevu, tuliomba wamuzuie kwanza nyumba kwake badala ya kumuweka gerezani moja kwa moja, majaji hawaku...

SERIKALI HUPOTEZA SHILINGI BILIONI 4 KWA AJILI YA KUAGIZA DAWA .

Image
WAZIRI WA AFYAMAENDELEO YAJAMII JINSIA WAZEE NA WATOTO UMMY MWALIMU   Timoth Marko  TAKRIBANI shilingi bilioni 4 hupotea kila mwaka  kutokana kuharibika kwa dawa zinazoagizwa nje yanchi kuja nchini TANZANIA hali inayochangiwa kutokuwepo kwa viwanda madhubuti ya uzalishaji dawa nchini. Akizungumza katika mkutano wa wawekezaji wenye nia yakuanzisha viwanda vya madawa nchini uliofanyika jijini Dar es salaam waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Ummy Mwalimu amesemakuwa  kutokana nakutokuwepo miundombinu mathubuti ya upokeaji dawa hali inayochangia dawa zinazoingia nchini kuisha muda wake nakusababishia hasara kubwa katika uagizaji wa dawa nchini . ''Tunapata changamoto ya uagizwaji wa dawa ikiwemo hali yakubadilika kwa thamani yadola kwa ajili ya kununua dawa ,hali hii hupelekea dawa nyingi kupoteza muda wake wamatumizi nakusababishia hasara serikali takribani shilingi bilioni nne katika kuagiza dawa nchini ''Alisema Waziri wa afya ummy...