TTCL Corporation kwa kushirikiana na tiGO Tanzania wazindua huduma ya kifedha (E-Money Joint)


1
Mkuu wa Kitengo cha TTCL Pesa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) Bw. Moses Alphonce (kulia) na Afisa Mkuu wa Kitengo cha Huduma ya Fedha Tigo Bw. Hussein Sayed wakipongezana kama ishara ya uzinduzi rasmi wa huduma za kifedha kwa jia ya mtandao katika ya TTCL Pesa na Tigo Pesa hafla hiyo imefanyika kwenye Ukumbi Golden Jubilee Tower (PSPF) jijini Dar es salaam leo.
2
Mkuu wa Kitengo cha TTCL Pesa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) Bw. Moses Alphonce (kulia) na Afisa Mkuu wa Kitengo cha Huduma ya Fedha Tigo Bw. Hussein Sayed wakipongezana kama ishara ya uzinduzi rasmi wa huduma za kifedha kwa jia ya mtandao katika ya TTCL Pesa na Tigo Pesa hafla hiyo imefanyika kwenye Ukumbi Golden Jubilee Tower (PSPF) jijini Dar es salaam leo, kulia ni Nasra Mugheiry Meneja Huduma na Maendeleo ya Bidhaa TTCL Pesa na kushoto ni Angelina Pesha Mkuu wa Kitengo cha Udhibiti wa Ubora Tigo Pesa.
3
Mkuu wa Kitengo cha TTCL Pesa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) Bw. Moses Alphonce akizungumza katika zunduzi huo.
04
Afisa Mkuu wa Kitengo cha Huduma ya Fedha Tigo Bw. Hussein Sayed akizungumza katika mkutano huo.
4
Mkuu wa Kitengo cha TTCL Pesa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) Bw. Moses Alphonce (kulia) na Afisa Mkuu wa Kitengo cha Huduma ya Fedha Tigo Bw. Hussein Sayed wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wenzao wa TTCL na Tigo mara baada ya uzinduzi huo.
………………………………………………………………………………………………
Na Stahmil Mohamed
Shirika la mawasiliano Tanzania TTCL limeingia makubaliano ya ushirikiano wa biashara na kampuni  ya simu za mikononi ya Tigo yatakayowezesha wateja wa taasisi zote mbili kubadilishana fedha na huduma za fedha kupitia simu zao za mkononi.
Hayo yamesemwa na mkuu wa Huduma za TTCL pesa Bw.Moses Alphonce katika ghafla ya kutangaza ushirikiano huo nakusema kuwa kwa kushirikiana na tigo pesa katika kuwapa wananchi suluhisho sahihi la mahitaji yao ya kifedha ikiwa ni kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya tano za kusogeza huduma karibu zaidi na wananchi.
Aidha Bw.Alphonce  amesema TTCL imeazimia kuwapa wananchi huduma za kiwango cha juu na cha ubora na unafuu wa gharama za kutuma ,kupokea na kufanya miamala kwa kutumia simu Zao hivyo wamedhamiria kubadili mifumo ya malipo yote ya umma na binafsi yafanyike kupitia mtandao ili kuongeza usalama na ufanisi wa shughuli za kiuchumi na kijamii.

Comments

Popular posts from this blog

Mvua yatatiza mpambano kati ya Simba SC na El Masri

Marubani Wawili Wapoteza Maisha kwa Ajali ya Ndege Zanzibar

Huduma za serikali ya Marekani zakwama kwa mara nyengine