JESHI LA POLISI LAWAONYA WATAKAO ANDAMANA APRIL 26

Tokeo la picha la MKUU WA OPERESHENI NA MAFUNZO WA JESHI LAPOLISI

 Kamishina Mkuu wa operesheni na mafunzo wa jeshi lapolisi nchiniTanzania Nsato Marijani

Timothy Marko

SIKU chache baada ya mwanaharakati anayeishi nchini Marekani Aliyenaasili ya Kitanzania Mange Kimambi kuwa hamasisha vijana na baadhi ya watu wenyerika mbalimbali kufanya maandamano 26 April mwaka huu kupinga utawala wa Rais wa Jamuhuri wa muungano wa Tanzania Dk.Jonh Pombe Magufuli ,Jeshi lapolisi limewataka wananchi kupuuza ujumbe wamwanaharakati huyo nakusisitiza kuwa jeshilo lipo makini halituruhusu Maandamano hayo kufanyika nchini kwani yanakiuka sheria za nchi.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es salaam Kamishina Mkuu wa operesheni na mafunzo wa jeshi lapolisi nchiniTanzania Nsato Marijani amsesema kuwa kitendo chakuipinga serikali inayongozwa na Rais wa Jamuhuri wa muungano wa Tanzania Dk.JOHN POMBE Magufuli kitendo hicho kinafananishwa na uhaini ambapo adhabu yake ni kunyongwa .

''Vijana wengi wameanza kuingia katika mkumbo huu ninawaomba vijana waache mkumbo huu kwani nihatari  lazima watanzania wafuate sheria za nchi nakuachana mikumbo kwani inaweza kuhatarisha amani namaisha yao kijumla ''Alisema Kamishina Nsato MARIJANI .

Comments

Popular posts from this blog

Mvua yatatiza mpambano kati ya Simba SC na El Masri

Marubani Wawili Wapoteza Maisha kwa Ajali ya Ndege Zanzibar

Huduma za serikali ya Marekani zakwama kwa mara nyengine