AFISA TRA AKUTWA NA TAKUKURU AKIDAI RUSHWA.

Tokeo la picha la pilly mwakasege

mkuu wa takukuru wilaya temeke pilly mwakasege

Timothy Marko
SIKU chache Baada ya Rais wa Jamuhuri wa Muungano wa Tanzania Dk. John Magufuli kuwatahadhalisha Maofisa wa Mamlaka ya kusanyajikodi nchini (TRA) Kutowalimbikizia kodi wananchi isivyo halali Taasisi ya kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU )wilayani Temeke jijini Dar es salaam inamshikilia Straton Mutayabrwa afisa wa TRA kata ya kigamboni baada ya kupokea Rushwa ya shilingi 300,000 kutoka kwa mwananchi ambaye jinalake limehifadhiwa ambaye ni mmiliki wa bucha kwa kosa lakutokuwa na mashine ya EFD.

Akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es salam Mkuu wa Taasisi yakupambana narushwa wilaya ya Temeke Pilly Mwakasege amesema kuwa mtuhumiwa huyo alitendakosa hilo februari 28 mwaka huu akimuomba miliki wa bucha hilo 30000 kwa kutokuwa na mashine za kieletroniki za efd ambapo mtuhumiwa huyo yupo nje kwa dhamana .
''KATIKA hatua nyngine Afisa wa ustawi wa jamii wa mahakama ya mwanzo ya buguruni alifikishwa mahakamani wilayani hapa nakufunguliwa kesi namba 136 /18wakati akiombarushwa yashilingi 300000nakuweza kupokea kiasi 20000 ili aweze kumsaidia ndugu yake alihukumiwa kifungo cha miezi nane jela naaweze kutumikia kifungo cha nje jela''alisema Pilly mwakasege .

Mwakasege alisema taasisi hiyo inawatadhalisha wananchi kutojihusisha navitendo vya rushwa kwani kutenda kosa hilo nikinyume  cha sheria yarushwa yanamba 11 ya mwaka 2007.

Comments

Popular posts from this blog

Mvua yatatiza mpambano kati ya Simba SC na El Masri

Marubani Wawili Wapoteza Maisha kwa Ajali ya Ndege Zanzibar

Huduma za serikali ya Marekani zakwama kwa mara nyengine