MBARAWA AWATAKA WAKANDARASI KUKAKAMILISHA MIRADI YA BARABARA KWA WAKATI

waziri wa ujenzi uchukuzi na mawasilano Profesa makame mbarawa  akizungumza na wakandarasi hawapo pichani jijini daes salaam leo


Timothy Marko.

SERIKALI imewataka makandarasi waliopewa miradi mbalimbali ya barabara kukamilisha miradi hiyo kwa wakati  huku wakitakiwa kuzingatia ubora wamiradi hiyo kama ilivyopangwa .

Wito huo umetolewa na waziri wa ujenzi uchukuzi na mawasiliano Professa Makame mbarawa jijini Dar  amesema serikali imeingia makubaliano hayo ya zaidi bilioni 702.5 katika kutekeleza miradi mbalimbali ya barabara ambapo fedha hizo zitatumika katika ujenzi wa barabara usesula hadi komanga yenye urefu km108 .

''Awamu yapili itajumuisha komanga hadi kisinde yenye urefu wakm 108 ikihusisha km4.8za barabara unganishi ya mji wa inyonga na mkandarasi aliyepatikana ni kampuni  ya china Wu yi  ambapo shilingi 140,025,481,457.00ikiwa nakodi ya ongezeko la VAT 18% ujenzi huu unatarajiwa kukamilika baada yamiezi 36''ALISEMA  profesa Makame mbarawa .

Profesa Mbarawa amesema kuwaawamu ya tatu ya ujenzi huo utajumuisha kashinde hadi mpanda ikihusisha km 2.29 za mji urwira ambapo mkandarasi aliyepatikana nikampuni yakutoka china kwa gharama ya  shilingi 133,803,828,397.29 ikiwa sasambamba nakodi ya asilimia 18.

Alisema kuwa awamu yanne yaujenzi huo utajumuisha ujenzi wa barabara yambinga  hadi mbambabay ambapo ujenzi huo utagharimu shilingi 129,361,352,517.84 sambamba navat ya asilimia 18.

Comments

Popular posts from this blog

Mvua yatatiza mpambano kati ya Simba SC na El Masri

Marubani Wawili Wapoteza Maisha kwa Ajali ya Ndege Zanzibar

Huduma za serikali ya Marekani zakwama kwa mara nyengine