Vijana watakiwa kutembelea makumbusho
Breaking News,
Habari
iliyoisha zikionyesha shughuli mbalimbali
walizokuwa wakizifanya ambapo hivi Sasa hazitiliwi mkazo hali yakuwa
zinafaida kubwa kwa Taifa kiujumla.
Na stahmil mohamed.
Vijana,wanafunzi wa shule za msingi na sekondari pamoja na vyuo wametakiwa kujijengea tabia ya kutembelea Makumbusho ili kujifunza na kuziendeleza fursa mbalimbali ambazo zilikuwa zinafanywa hapo awali ili kujipatia kipato na kukuza uchumi wa nchi.
Vijana,wanafunzi wa shule za msingi na sekondari pamoja na vyuo wametakiwa kujijengea tabia ya kutembelea Makumbusho ili kujifunza na kuziendeleza fursa mbalimbali ambazo zilikuwa zinafanywa hapo awali ili kujipatia kipato na kukuza uchumi wa nchi.
Hayo yamesemwa na mkurugenzi wa Makumbusho Bw.Audax mabula
alipokuwa akizungumza katika maonyesho ya picha ya "Karibu
Tanzania"yaliyofanyika Makumbusho ambapo amewataka vijana kutembelea
Makumbusho ambapo wataweza kujifunza vitu mbalimbali kupitia picha
ambazo zilipigwa miaka 50
Hata hivyo Bw.Mabula ameongeza kwa kusema kuna umuhimu
mkubwa kwa vijana wa nchi hii kufatilia mambo yaliyofanywa hapo awali
kama kufinyanga,kuchonga na kutengeneza dhana mbali mbali kwa ajili ya
kilimo ili kujikwamua kiuchumi hivyo kupitia jumba LA maonyesho LA
Makumbusho ya Taifa wataweza kujifunza hivyo vyote pia wataweza kuzijua
asili zao kiundani kwani wataweza kujifunza tamaduni za kwao kwa kutumia
picha mbalimbali zilizopo hivyo kuna haja kubwa ya kutembelea
Makumbusho.
Kwa upande wake balozi wa Denmark ambae alikuwa mgeni rasmi
katika onesho hilo LA picha Bw.Einar.H.Jensen amesema kuna haja kubwa
ya kujifunza vitu vinavyohusiana na asili zetu kwani vina tija hivyo
amewaasa vijana zaidi kutembelea makumbusho kujifunza kwa nadharia kwani
wao ndio muhimili mkubwa katika kila Taifa.
Pia kwa upande wa baadhi ya wanafunzi waliohudhuria katika
onesho hilo waliotokea shule ya Baobab wamefurahi kushiriki katika
onesho hilo kwani wamejifunza vitu vingi ikiwemo kuona namna watu wa
zamani walivyokuwa wakijikwamua kiuchumi kupitia shughuli za
kilimo,uhunzi na vinginevy
Comments
Post a Comment