NECTA YAWATADHALISHA WAMILIKI WASHULE JUU YA VITENDO VYA UDANGANYIFU.

Image result for charles msonde

 Katibu wa Baraza la Mitihani la taifa NECTA  Dk.Charles Msonde 

Timothy Marko.
BARAZA la Mtihani la Taifa (Necta) limewataka wasimamizi walimu na watahiniwa pamoja na wamiliki wa shule za Msingi kutojihusisha navitendo vya udanganyifu katika mtihani wa Darasa la Saba unaotarajiwa kuanza kesho .

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam Katibu wa Baraza hilo Dk.Charles Msonde amesema kuwa Baraza hilo halitasita kumchukulia hatua mtu yeyote atakayejihusisha na udanganyifu katika mitihani itakayofanyika kwa siku mbili kuanzia tarehe 6na 7 september mwaka huu kwani nikunyume cha sheria za nchi .
''watahiniwa watakao bainika kufanya vitendo vya udanganyifu watafutiwa matokeo yote kwa mujibu wa kanuni za mtihani ninawataka wadau kutoa taarifa katika vyombo husika kila wanapobaini kikundi chochote kinajihusisha navitendo hivyo ''Alisema Dk.Charles Msonde .

Katibu wa Baraza la Mtihani Msonde alisema kuwa katika kipindi cha mwaka huu jumla ya watahiniwa 917,072 wanatarajiwa kufanya mtihani huo kesho ambapo kati yao wavulana 432,744 sawa na asilimia 47.9 wakati wasichana 484,328 wanatarajiwa kufanya mtihani huo kote nchini .
Alisema msomo yatakayo tahiniwa katika mtihani huo nipamoja na kiswahili English SANYANSI ,hisabati na maarifa ya jamii.

Comments

Popular posts from this blog

Mvua yatatiza mpambano kati ya Simba SC na El Masri

Marubani Wawili Wapoteza Maisha kwa Ajali ya Ndege Zanzibar

TANZANIA KUWA MWENYEJI WA CHANGAMOTO ZA MADAWATI YAKIJINSIA JUNE 13