MAUZO YA HISA JIJINI YAFIKIA BILIONI 53.5

Timothy Marko.
 KIWANGO cha mauzo  ya hisa katika soko la hisa la Dar es salaam (DSE)kimeongezeka kutoka shilingi bilioni 5.4 wiki iliyopita hadi kufikia shilingi bilioni 53.5 mnamo September 22 mwaka huu .

AFISA MWANDAMIZI WA SOKO LA HISA DSE MARY KINABO AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI LEO JIJINI DAR ES SALAAM

Kuongezeka kwa mauzo ya hisa hizo kumetokana na kuongezeka kwa ukubwa wa mtaji katika kampuni ya Kenya Airways kwa asilimia 20 pamoja na uchumi super market kwa asilimia 12.5pamoja benki ya kibiashara ya Kenya kuongezeka kwa asilimia 9.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam Afisa mwandamizi wa Soko la hisa soko hilo jijini dar es salaam Mary kinabo amesema kuwa ukubwa wamtaji wa kampuni zandani umeongezeka kutoka shilingi milioni 27 hadi kufikia shilingi trioni 9.5

‘’Makapuni yaliyo ongoza wiki hii katika mauzo ya hisa nipamoja na Benki ya biashara ya CRDB ,DCB Pamoja na Soko lahisa la Dar es salaam’’Alisema Mary kinabo

Afisa Mwandamizi wa soko la hisa Kinabo alisema kuwa wakati mauzo ya hisa ya  kiongezeka kutoka bilioni 5.4hadi kufikia shilingi trioni9.5 mauzo ya hati fungani hadi kufikia September mwaka huu yameongezeka kutoka bilioni 22 hadi kufikia bilioni 36.


Alisema kuwa kiashiria cha kampuni za ndani TSI kimepanda kutoka pointi 11 kutoka 3.704 hadi pointi 3,715. 

Comments

Popular posts from this blog

Mvua yatatiza mpambano kati ya Simba SC na El Masri

Marubani Wawili Wapoteza Maisha kwa Ajali ya Ndege Zanzibar

Huduma za serikali ya Marekani zakwama kwa mara nyengine