MAKONDA AWATAKA WANANCHI KUHESHIMU MAENEO YALIYOTENGWA KWA MAPUMZIKO.

Image result for makonda tanzania
MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM PAUL MAKONDA

Timoth Marko
Mkuu wa mkoawa jiji laDar es salaam  Paul Makonda  amewataka kwa wakazi wa jiji hilo,kutunza na kulinda mazi ngira ya bustani ya kaburi moja iliyopo maeneo ya samora katika wilaya ya ilala,  katika uzinduzi wa bustani hiyo ambayo ilijengwa kwa kiasi cha fedha za kimarekani dola 380,000 lengo la eneo hilo ikiwa  ni kwa ajili ya wananchi kupumzika.


Makonda ameyasema hayo leo katika uzinduzi wa eneo hilo, ambapo Mh. Makonda amekata utepe katika bustani hiyo, ilifanyiwa marekebisho na matengenezo na wadau wa JAICA, wakiwa na lengo la  kuijenga dar es salaam mpya, ambayo imeleta muonekano mpya na ni faida kwa wananchi wote watakaotumia sehemu hiyo. Na pia amewataka wafanya biashara wodogo wadogo(wamachinga) kutokufanya biashara katika eneo hilo.

"Eneo letu hili siyo la kufanya biashara kwa ndugu zetu (wamachinga) ni eneo La watanzania wote wanaoitaji  kupumzika, tumepajenga ili wananchi wote hatujajenga ili kufanya biashara la hasha! Hili ni eneo la kupumzika kwa mtu yeyote anaehitaji kupumzika baada ya kufanya shughuli zao wengine watapumzika  kusubiri magari au mtu anaetaka kujiliwaza anaruhusiwa kupumzika katika bustani hii" Alisema Makonda.

Hata ivyo ameongeza kuwa katika kuboresha maeneo yote ya jiji vituo vya daladala vitafanyiwa marekebisho, ambapo vituo hivyo vikijengwa upya na kuboresha itakuwa ni sehemu nzuri ya kuweka matangazo,na kumjenga jiji hilo na  lengo la dar es salaam mpya itatimia.


Comments

Popular posts from this blog

Mvua yatatiza mpambano kati ya Simba SC na El Masri

Marubani Wawili Wapoteza Maisha kwa Ajali ya Ndege Zanzibar

TANZANIA KUWA MWENYEJI WA CHANGAMOTO ZA MADAWATI YAKIJINSIA JUNE 13