KAMISHINA MUSILIMU AWATAKA KIKOSI CHA USALAMA BARA BARANI KUZINGATIA SHERIA .

Tokeo la picha la fotunatus musilimu

mkuu wa kikosi cha usalama barabarani  Kamishina Musilim 

Timoth Marko

MKUU wa Kikosi cha usalama barabarani nchini Tanzania Fotunatus Musilim amewataka jeshi la polisi  wakikosi cha usalama barabarani kuzingatia sheria pindi jeshi hilo linapowakamata madereva wa bodaboda nakuachana na tabia ya kuwapiga madereva hao pindi wanapo kiuka sheria nabadala yake wakamamatwe nakuweza kufikishwa mahakamani ilikuweza kujibu tuhuma zinazo wakabili .

Akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es salaam Kamishina Musilim amesema kuwa kwamujibu washeria za jeshi hilo limepewamamlaka ya kuwakamata wahalifu kwa mujibu wa sheria lakini jeshi hilo halirusiwikumpiga raia lakini linatakiwa kumuandikia notification ama maelezo yakumpeleka mahakamani nasio kupiga raia .

''Hakuna sheria katika nchi hii inayoruhusu kupiga mtu yoyote mtu anapotenda kosa anapelekwa mahakamani asante kwakunitarifu kwa jambo hili nitalifuatilia nijue ukweli kuhusiana na jambo hili kwa mujibu wa sheria jeshi lapolisi limepewa mamlaka kuwakamata wahalifu lakini nikwamujibu washeria nasio vinginevyo ''Alisema Kamishina Musilim

Kamishina Musilimu alisema kuwa sheria imetoa msamaha kwa magari yaviongozi pindi yanapokuwa katika msafara sambamba namagari yote ya vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na magari yadharua pindi wanapotumia bara bara katika shughuli zao .

Alisema sambamba nakutoa msamaha kwa magari hayo pia zipo sheria ndogo ndogo zinazotumiwana manispaa katika kumkamta mtu yeyote anaye kiuka sheria za barabarani .

Comments

Popular posts from this blog

Mvua yatatiza mpambano kati ya Simba SC na El Masri

Marubani Wawili Wapoteza Maisha kwa Ajali ya Ndege Zanzibar

Huduma za serikali ya Marekani zakwama kwa mara nyengine