PONDAMALI AWAAMBIA SIMBA WASUBIRI SASA BAO LA TAMBWE
Ikiwa
ni siku mbili baada ya kutoa sare ya bao 1-1, Kocha wa Makipa wa Yanga,
Juma Pondamali ‘Mensah’, amefunguka na kudai kuwa ligi haijaisha na
watalipa kisasi tu na kuhakikisha wanawafunga Simba, lakini kocha huyo
amedai kuwa Simba wana bahati kwa kuwa Amissi Tambwe na Donald Ngoma
hawakuwepo.
Juzi
Jumamosi Yanga iliwakosa baadhi ya mastraika viwembe wa timu hiyo
akiwemo Amissi Tambwe na Donald Ngoma ambao wamekuwa na rekodi safi ya
upachikaji mabao.
Katika
mchezo huo, bao la Yanga lilifungwa na straika Mzambia, Obrey Chirwa
ambapo mpaka sasa tayari amefikisha mabao matatu msimu huu lakini
Emmanuel Martin alikosa nafasi adimu ambayo ingeweza kuipa ushindi
Yanga.
Kocha
huyo alisema mchezo huo ulikuwa na ushindani ingawa wao walipata nafasi
nyingi na walishindwa kuzitumia vyema na kusababisha kuambulia alama
moja.
“Juzi
Simba wamelipata bao la Chirwa tu mzunguko ujao litakuwepo la Tambwe,
Ngoma, Ajibu yaani watabaki kuhesabu maana hatutawapa nafasi tena ya
kutufunga wajue kabisa.
“Tumepata
pointi moja ila tumewakosa mengi lakini tunajipanga, Simba wajiandae
kabisa kisaikolojia kwa sababu tukikutana tena wataishia kuhesabu mabao
tutahakikisha kila mshambuliaji wetu anafunga na kupata ushindi wa
nguvu,” alisema Pondamali.
Ikiwa
ni siku mbili baada ya kutoa sare ya bao 1-1, Kocha wa Makipa wa Yanga,
Juma Pondamali ‘Mensah’, amefunguka na kudai kuwa ligi haijaisha na
watalipa kisasi tu na kuhakikisha wanawafunga Simba, lakini kocha huyo
amedai kuwa Simba wana bahati kwa kuwa Amissi Tambwe na Donald Ngoma
hawakuwepo.
Juzi
Jumamosi Yanga iliwakosa baadhi ya mastraika viwembe wa timu hiyo
akiwemo Amissi Tambwe na Donald Ngoma ambao wamekuwa na rekodi safi ya
upachikaji mabao.
Katika
mchezo huo, bao la Yanga lilifungwa na straika Mzambia, Obrey Chirwa
ambapo mpaka sasa tayari amefikisha mabao matatu msimu huu lakini
Emmanuel Martin alikosa nafasi adimu ambayo ingeweza kuipa ushindi
Yanga.
Kocha
huyo alisema mchezo huo ulikuwa na ushindani ingawa wao walipata nafasi
nyingi na walishindwa kuzitumia vyema na kusababisha kuambulia alama
moja.
“Juzi
Simba wamelipata bao la Chirwa tu mzunguko ujao litakuwepo la Tambwe,
Ngoma, Ajibu yaani watabaki kuhesabu maana hatutawapa nafasi tena ya
kutufunga wajue kabisa.
“Tumepata
pointi moja ila tumewakosa mengi lakini tunajipanga, Simba wajiandae
kabisa kisaikolojia kwa sababu tukikutana tena wataishia kuhesabu mabao
tutahakikisha kila mshambuliaji wetu anafunga na kupata ushindi wa
nguvu,” alisema Pondamali.
0 COMMENTS:
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.