SERIKALI KUBORESHA HUDUMA YA MAJI JIJINI DAR ES SALAAM.
MAKAMU WA RAIS WA JAMUHURI YAMUUNGANO WA TANZANIA SAMIA HASSAN |
Timothy Marko .
SERIKALI imesema itaendelea kuboresha sekta ya maji katika miji mikuu kutoka asilimia 86 hadi kufikia asilimia 95 ambapo imebainisha kuwa hadi kufikia 2020 hali upatikanaji wa huduma hiyo inatarajiwa kuongezeka kutoka asilimia 72 hadi kufikia asilimia 95.
Kauli hiyo imetolewa naMakamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano waTanzania Samia Suluhu jijini Dar es salaam wakati akizindua mpango mkakati wa water aid uliondaliwa nawizara yamaji na umwagiliaji ambapo amesema kuwa Hatua yakuongeza hudumahiyo yamaji itahusisha wadau mbalimbali wasekta hiyo pamoja na serikali .
''Sambamba nahilo serikali itaendelea kusisitiza suala lausafi wa mazingira ilikuweza kuhakikisha tunalinda afya zetu ilitusishambuliwe na magonjwa yamlipuko kama vile kipindupindu na homa yamatumbo ''Alisema Makamu wa Rais Samia suluhu .
Makamu wa Rais Suluhu alisema kuwa mpango huo ambao unalenga kuweka maji safi namazingira ni agenda muhimu ya maendeleo kama ilivyopendekezwa katika mpango wa awamu yapili ujulikanao kama WSP II 2016-2021 ikiwa nidira yamaendeleo ya taifa ya mwaka 2025.
Comments
Post a Comment